MBUNGE WA PANGANI AENDELEA NA ZIARA WILAYANI HUMO



Mbunge wa Jimbo la Pangani Mheshimiwa Jumaa Hamidu Awes leo ameendelea na ziara yake katika jimbo lake na kutoa msaada wa Mifuko arobaini ya saruji katika shule ya chekechea ya Childrens Of Choba wilayani humo.

Akizungumza wanafunzi na viongozi wa shule hiyo mbunge Jumaa amesema kuwa ameamua kutoa mifuko arobaini ya Saruji kutokana na kutambua mchango wa meneja wa shule hiyo katika kuendeleza watoto wa Pangani katika elimu.

Kwa upande wake Meneja wa  shule hiyo Bi Valeri Makgiven ameshukuru kwa msaada huo akisema utasaidia katika kupanua ujenzi wa madarasa ya Awali katika shule hiyo.

Hata hivyo baadhi ya wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo wamemshukuru Mbunge huyo kwa msaada alioutoa huku wakimuahidi watajihidi katika kujisomea ili waweze kupata mafanikio kielimu. 

Mbunge wa jimbo la Pangani mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso bado anaendelea na Ziara yake kutembelea vijiji vya jimbo hilo ili kutambua changamoto zilizopo na kuzitatua kabla ya kurudi bungeni  mwezi wa Tisa mwaka huu.

No comments

Powered by Blogger.