VMAC KIJIJI CHA LANGONI WATOA MAHINDI KWA AJILI YA CHAKULA SHULENI



Kamati ya kudhibiti UKIMWI jinsia na Uongozi VMAC kijiji cha Langoni wilayani Pangani leo wametoa msaada wa mahindi Kilo mia tatu pamoja na Pesa taslimu shilingi elfu thelathini katika shule ya msingi ya kijiji hicho kwa ajili ya kufanikisha upatikanaji wa chakula shuleni hapo.

Akizungumza wakati wa zoezi la Utoaji wa Msaada huo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bi IMANI BAKILI amesema kuwa wameamua kutoa msaada huo kutokana na kuwawezesha wanafunzi wa shule hiyo kupata chakula wakiwa shuleni ili kusaidia uwelewa mzuri wa masomo kwa wanafunzi hao.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Langoni Mwalimu MOHAMEDI SALUM ameishukuru kamati hiyo kwa kutoa msaada huo kwani utasaidia kutatua changamoto ya chakula kwa wanafunzi  pamoja na kambi ya wanafunzi wa darasa la saba wanaojiandaa kufanya mtihani.

Nao baadhi ya wanafunzi  wa shule hiyo wameelezea kufurahishwa na msaada huo wa mahindi uliotolewa na kamati hiyo kwani itasaidia, kwa kuwa kuna baadhi wanafunzi wenzao ambao hutembea umbali mrefu hadi kufika nyumbani wakiwa na njaa.

Hii inajumuisha shughuli mbalimbali za kujitolea zilizofanywa na Kamati hiyo ya VIMAC ya kijiji cha Langoni ndani ya mwaka huu ambapo hivi karibuni walijitolea kuchimba msingi wa kupitishia mipira ya maji katika kijiji chao.

No comments

Powered by Blogger.