VMAC YA KIJIJI CHA MWEMBENI YATOA MSAADA WA VIFAA VYA HUDUMA YA KWANZA MASHULENI



Kamati ya kudhibiti Ukimwi Jinsia na Uongozi ya kijiji cha MWEMBENI leo imetoa msaada wa vifaa vya Huduma ya Kwanza katika shule za Sekondari ya Bushiri na Boza pamoja na shule za msingi Mwembeni na Madanga ikiwa ni mchango wao katika kuendeleza gurudumu la elimu.

Akizungumza na Pangani fm mwenyekiti wa kamati hiyo Bi PILI YUSUFU amesema  kuwa lengo la kutoa msaada huo wa chakula pamoja na vifaa vya huduma ya kwanza ni kusaidia upatikanaji wa chakula katika shule hizo na kusaidia utolewaji wa huduma ya kwanza endapo mwanafunzi atapata ajali.

Kwa upande wa walimu wa shule hizo zilizopata msaada wa chakula na vifaa hivyo wameishukuru sana kamati hiyo kwa mchango wao wakielezea kwamba utawasaidia kwa kiasi kikubwa kwani umefika kwa wakati muafaka.

Kamati hiyo pia imetoa mahindi kilogram 100, Mchele kilogram 30 vifaa vya huduma ya Kwanza kwa shule ya msingi Mwembeni, Mahindi gunia 1 na vifaa vya huduma ya Kwanza kwa shule ya sekondari bushiri huku shule ya Msingi Madanga na Sekondari Boza zikipatiwa vifaa vya huduma ya kwanza pekee.

No comments

Powered by Blogger.