WAITARA ATEMA CHECHE PANGANI


Naibu Waziri ofisi ya Rais TAMISEMI mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara ameagiza kusimamishwa kazi afisa mipango wa halmashauri ya wilaya ya PANGANI Bwana Waziri Mwakibolwa kutokana na kusua sua kwa utendaji wake.

Naibu waziri Mwita amesema Hayo kupitia ziara ya siku moja aliyoifanya wilayani pangani wakati akizungumza na watumishi wa halmashauri hiyo yenye lengo la kuangalia tathimini ya utendaji kazi baada ya kutembelea baadhi ya shule za serikali. 

Amesema Kusimamishwa kazi kwa Bwana Mwakibolwa kumetokana na malalamiko mbali mbali ikiwemo utendaji kazi mbovu, ukosefu wa nidhamu, ulevi huku akiwataka viongozi wa halmashauri kutoa taarifa kama wanaupungufu wa watendaji.

 ’Kwa hiyo huyu asimamishwe kazi mara moja kutokana na malalamiko dhidi yake na sio leo ana mengine ya utovu wa nidhamu na watu wameshaleta taarifa nyingi tofauti na hizo za mkuu wa mkoa, natambua kuna taarifa nyingi kule ofisini kwamba hapa kuna shida ya afisa mipango, kama kuna shida ya upungufu wa watumishi hapa ije ajenda maalumu ya kiofisi.’’ 


Mheshimiwa Waitara pia amekemea tabia za viongozi kuwarudisha kazini watumishi waliosimamishwa kazi bila ya kufuata taratibu za kisheria huku akimtaka kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bwana Daudi Mlahagwa kuandika barua ya kuomba radhi kutokana na kukiuka maamuzi ya ngazi za juu na kumrudisha kazini Bwana Mwakibolwa ambaye alisimamishwa kazi na mkuu wa mkoa wa tanga Bwana Martin Shigela.
‘’Ili mtu arudushwe kazini ni lazima timu ifanyie kazi, kwamba hizi taarifa ambazo tunazo kama ni chuki, ni husda vyote vinatakiwa vijulikane, kwa hiyo hii habari ya kuwatumia madiwani kuja kujiridhisha watu ambao wanalalamikiwa na kufanya mkuu wa mkoa aje aonekane kuwa hamna kitu, kwa sababu anatoa maagizo alafu watu wanakuja kuyapinga, na huyu kaimu mkurugenzi anatakiwa kuandika barua ya kuomba radhi kwa kukiuka maagizo ya ngazi ya juu”



Awali mkuu wa mkoa wa tanga Bwana Martin Shigela alimuagiza aliyekuwa kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Pangani Bwana Daudi Mlahagwa kumsimamisha kazi afisa mipango wa halmashauri ya hiyo Bwana Waziri Mwakibolwa kutokana na malalamiko yaliyotolewa kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichojadili kutotumika kwa fedha za mfuko wa jimbo hadi kuvuka mwaka bila ya matumizi hali ya kuwa wananchi wanauitaji nazo.




No comments

Powered by Blogger.