WANANCHI PANGANI WATAKIWA KUFUATA TARATIBU ZA KUTOA USHAHIDI


Wananchi wilayani Pangani wametakiwa kufuata utaratibu na kutoa na taarifa katika jeshi la Polisi sambamba na kutunza eneo la ushahidi panapotokea tukio ambalo litakalowezesha kubaini na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa muhusika.
Akizungumza kwa niaba ya Kamanda wa jeshi la Polisi wilayani humo Afande Kenethy Matondwa amewataka wanajamii kuacha kushika vielelezo vinavyopatikana eneo la tukio ili kutunza ushahidi utakosaidia kupatikana kwa haki stahiki itakayopelekea  kupunguza matukio uhalifu miongoni mwajamii.
‘’Nawasihi na kuwaomba sana wanajamii ya Pangani na kokote pale wanaotusikiliza tubadilike kutoka kwenye ile dhana sasa ya kuwa na haraka hivyo ukashika kama ni kisu ni silaha au ni nini ukasema uonekane kwa polisi kuwa umefanya vizuri zaidi kumbe umeharibu zaidi, kwa hiyo badala yake tufuate utaratibu na maelekezo haya ambayo nayatoa kwamba ni kitu umeshuhudia kibaya unakitazama kwa macho na toa taarifa kwa ngazi ya kijiji, kata, jeshi la polisi wafike na wafanye taratibu zao za kiupelelezi ‘’ amesema bwana Kenneth.
Akizungumzia kuhusu hofu ya wananchi kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pindi wanaposhudia miili ya marehemu kwa kuhofia kushikiliwa na jeshi hilo ili kusaidia upelelezi Bwana Matondwa amesema..
‘’Dhana hii ni potofu kabisa na kwamba haipaswi kuwepo vichwani kwa wanajamii wetu na badala yake waiondoe mara moja waisaidie polisi au serikali kwa ujumla kwa kutoa taarifa hizi, hakuna askari polisi ambaye ataweza kukukamata wewe kwa kuwa umetoa taarifa ya kuonekana kwa mwili wa mtu aliyepoteza maisha’’ ameongeza Bwana Keneth.
Hayo yamejiri katika kipindi cha Asubuhi Ya Leo wakati wa kujadili hoja ya umuhimu wa kutunza  ushahidi katika eneo la tukio.


No comments

Powered by Blogger.