BODA BODA FC YAENDELEZA UBABE KWA CHELSEA YA BOZA



Ligi ya  AWESSO CUP inayoendelea kurundima  katika  kijiji cha Boza wilayani Pangani, imetimua vumbi katika viunga vya Uwanja wa mpira  shule ya msingi Boza, katika mchezo uliowakutanisha Boda Boda Fc na Chelsea ya Boza.

Mpaka dakika tisini ya mchezo Boda Boda imewacharaza bao 2 kwa 1 timu y Chelsea fc, mabao ya timu ya Boda boda yamewekwa kimiani na Ngongo Mbwana mnamo dakika ya 61 Na Seiph Mwakijo Dakika ya 84 huku bao la kufutia machozi la timu ya Chelsea likifungwa na Juma Bakary.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa mchezo unaowakutanisha RENGERS STAR ya mwembeni na CHOBA STAR ya choba.

No comments

Powered by Blogger.