ULEVI WA KUPINDUKIA UMEELEZWA KUWA NI CHANZO CHA UDHALILISHAJI NA UKATILI KWA WANAWAKE



Ulevi Wa kupindukia umeelezwa kwa chanzo kinachosababisha udhalilishaji na ukatili kwa wanawake hasa katika maeneo ya vijijini.
Licha ya udhalilishaji kujitokeza pale ambapo mwanamke mwenyewe anakwenda kilabuni na kulewa hadi kufikia hatua ya kutojitambua na kujikuta akifanyiwa vitendo vya kikatili kama kuliwa mande, vitendo vitendo ambavyo vimekuwa vikijitokeza sana katika maeneo ya vijijini.

Bi Adelina Rajabu ambae ni mkazi wa kijiji cha Kigurusimba Wilayani Pangani ni miongoni mwa wale waliowahi kupigwa na mumewe huku chanzo akieleza kuwa ni ulevi.

Bi Adelina ameieleza Pangani fm kwamba mara nyingi mumewe anapokuwa amelewa amekuwa akimtoloea maneno ya kumsimnga na kumtaka arudi nyumbani kwao, licha ya kuwa baada ya mumewe kumtolea maneno hayo amekuwa akifungasha mabegi na kujibanza pembeni na nyumba yake kwa lengo la kusubiri mumewe apunguze hasira kisha kurudi nyumbani kwake na kuendelea kuwepo nyumbani hapo.

Pamoja na mume wa Adelina kuwa na tabia ya masimango kila amapolewa sasa imefikia hatua ya kumchapa mkewe kwa fimbo kama mtoto hali iliyopelekea Bi adelina kupata maumivu makali mwilini wake, lakini kwa sasa Bi Adelina ameamua kurudi nyumbani kwa wazazi wake ili apumzike.


Mama mzazi wa Adelina BI MWAJUMA DAUDI ameeleza kusikitishwa na tukio hilo na kuchukua hatua ya kutoa taarifa kwenye uongozi wa kijiji.

Bi Mwajuma amewataka wanaume wote wenye tabia ya kuwapiga au kuwafanyia vitendo vya kikatili wanawake kuacha tabia hiyo kwani kufanya hivyo ni kushusha thamani na hadhi ya mwanamke.

Licha ya BI ADELINA kumsamehe mumewe kwa kitendo cha kumchapa kwa sasa ameamua kuishi nyumbani kwa wazazi wake hadi pale maumivu yatakapoisha


No comments

Powered by Blogger.