MWANAMKE AENDA JELA KWA KUPATIKANA NA HATIA YA KUOLEWA MARA MBILI



Mahakama ya  mwanzo ya Mwera imemuhukumu Asha Hassani mwenye umri wa miaka 32 mkazi wa Langoni, kwenda jela miezi 9 ama kulipa  faini ya shilingi laki 5 baada ya kupatikana na hatia ya kuolewa mara mbili.

Akisoma hukumu hiyo hakimu wa mahakama ya mwanzo ya Mwera Anthon Hamza  amesema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo la kuolewa na mwanaume mwingine huku akifahamu kwamba yeye ni mke wa mtu kutokana na ndoa yake na mumewe wa kwanza ikiwa bado haijavunjika.

Katika hati ya mashataka iliyowasilishwa na polisi mahakamani hapo ilidaiwa kuwa mnamo tarehe 29 mwezi wa 5 majira ya saa mbili na nusu usiku huko Langoni Bi Asha  aliolewa na Bwana DUNGU OMARI, ambapo mwanzo kabla ya hapo alikuwa ameolewa na Bwana DOTTO JUMA, na hii ilikuwa ni tarehe 5 mwezi wa 5 mwaka 2002 ndoa iliyofungishwa na Sheikh Mohamed Ally Muhaka.

Kutokana na ndoa ya awali kuwa bado haijavunjika  kwa hati ya talaka kwa mujibu wa sheria za kiislamu basi imeonekana ni kosa kwa Bi ASHA HASSANI kuolewa hali ya kuwa alikuwa bado ni mke wa mtu kisheria, na baada ya hukumu hiyo mtuhumiwa huyo alishindwa kulipa faini hiyo hivyo kwenda jela miezi hiyo tisa. 

Mahakama hiyo pia imemuhukumu Bwana Twaha Rajabu mkazi wa mkalamo mwenye umri wa miaka 23 kwenda jela miezi mitano au kulipa faini ya shilingi laki tatu na nusu, baada ya kupatikana na hatia ya kumtishia mtu kwa silaha aina ya sime.

Katika hati ya mashataka iliyowasilishwa na polisi mahakamani hapo ilidaiwa kuwa mnamo tarehe 8 mwezi wa 8 majira ya saa moja huko  Mkalamo Bwana Twaha alimtishia Bwana Jumanne Juma kwa sime,na baada uendeshwaji wa kesi hiyo mahakama ilimkuta na hatia kijana Twaha Rajabu,ambapo alishindwa kulipa faini hiyo ya shilingi laki tatu na nusu na kwenda kutumikia kifungo hicho cha miezi mitano gerezani.

No comments

Powered by Blogger.