VMAC YA KIJIJI CHA MIVUMONI YATOA MCHELE KWA SHULE YA MSINGI



Kamati ya kudhibiti Ukimwi ya kijiji cha Mivumoni hii leo imetoa Msaada wa  mchele Kilo 23 kwa wanafunzi wa Darasa la saba shule ya msingi Mivumoni  kama chachu ya kufanya vizuri katika mitihani yao ya mwisho.

Akizungumza na Pangani fm wakati akikabidhi chakula hiko , mwenyekiti wa kijiji hiko Bwana Venasi Onesmo amesema kuwa lengo la kutoa chakula hiko ni kuwapa motisha wanafunzi hao kujifunza zaidi hali itakayopelekea kujiaanda vyema na mitihani.

Mbali na kugawa mchele huo, kamati hiyo pia imeanza ujenzi wa choo katika ufisi ya kijiji cha Mivumoni kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri.
Kwa upande wao wanafunzi wa darasa la saba wa shule hiyo wameshukuru kwa kupewa mchele na kuahidi kufanya vizuri katika mitihani ya mwisho.

Naye mwalimu mkuu wa shule hiyo Ndugu Kalage Zahoro licha kutanabaisha kuwa tangu waanze kambi  ya masomo ratiba yao ilikuwa ugali na mapure,Pia ametoa shukrani kwa msaada huwo wa chakula huku akisema matumaini yake wanafunzi hao kufanya vyema.

Kamati za kudhibiti ukimwi zinazoratibiwa na shirika lisilo la kiserikali uzikwasa zimekuwa zikichangia  misaa mbali mbali katika shule za msingi na sekondari wilayani pangani kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu wilayani pangani.

No comments

Powered by Blogger.