HATIMAE JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI LAZINDULIWA PANGANI



Wanawake Wilayani Pangani wamefanya hafla ya kuzindua jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi kwa kupiga kura iliyowezesha kuwapata viongozi watakao wawakilisha katika  jukwaa hilo.

Jukwaa hilo linalenga kuwakutanisha wanawake ,kujadili fursa,changamoto na  na jinsi ya kushiriki kikamilifu katika biashara  na shughuli nyengine za uchumi ,vilevile kuongeza uwelewa wa wanawake hao katika masuala ya kiuchumi.

Waliochaguliwa kuwa viongozi wa jukwaa hilo ni Bi Manusa Bakari kwa nafasi ya mwenyekiti, na BI Fatuma Issa kwa nafasi ya makamu mwenyekiti.


Katibu ni Bi Akida Sabiri Masanga,na katibu msaidizi ni Bi Mwantumu Makuka.

Mweka hazina ni Bi Hawa Kizamba

Wajumbe wa kamati tendaji ni ;-
1.    Matingisa Hamza
2.    Mwanasha Rajabu
3.    Priscar Zakari
4.    Mwantumu Rajabu
5.    Mwanaidi Omari

No comments

Powered by Blogger.