VMAC YA KIJIJI CHA MSARAZA WILAYANI PANGANI YATOA MSAADA



Kamati ya kudhibiti Ukimwi, Jinsia na Uongozi ya kijiji cha Msaraza imepongezwa kwa kazi ya kutoa elimu, kuchangia chakula pamoja na kuhamasisha jamii katika shughuli za kimaendeleo katika kijiji chao.

Akizungumza na wananchi waliohudhuria tamasha lililoandaliwa na wajumbe wa VMAC wa kijiji hicho mgeni rasmi Bwana Daudi Mlahagwa ambae ni kaimu mkurugenzi wilaya ya Pangani amesema  kamati hiyo imefanya kazi kulingana na mafunzo waliyoyapokea kutoka shirika la UZIKWASA.

‘’Kuna mambo mengi sana ambayo mnayafanya vimac ya kijiji hichi cha Msaraza, mmeweza kutoa elimu kwa wanakijiji, mmeweza kutoa chakula kwa wanafunzi wa shule, mmeweza kuhamasisha jamii kwa ajili ya ushiriki wao katika shughuli za maeneleo, na kupiga vita unyanyapaa na maambukizi ya ukimwi lakini naamini haya yote ni kwa kushirikiana na shirika la uzikwasa pia nichukuwe fursa hii kulipongeza shirika hili kwa kazi nzuri ya kuzipa nguvu kamati za vimac.’’ Mlahagwa.




Kwa upande wa madiwani waalikwa kwenye Tamasha hilo Mheshiwa John Semkande pamoja na Bi Samira Kassim wamesema wako tayari kuiunga mkono kamati hiyo pamoja na kumtaka mkurugenzi wa halmashauri kuwashika mkono katika shughuli za kimaendeleo.

‘’jamani nafarijika sana kwa sababu mwenyekiti mwenzangu wa kijiji ni wa chama cha demokrasia na maendeleo kwa hiyo niwaambie tu kwamba maendeleo hayana chama, kwa hilo tutaungana na nyinyi kwa kutoa zawadi ya mbuzi mmoja’’ amesema Mheshimiwa Semkande.   



Naye katibu wa kamati hiyo Bwana Iddi Waziri Mazika amesema kuwa wametoa zawadi kwa watoto yatima wazee na bima kwa wanafunzi 60 wa shule za msingi.

‘’Kutoa zawadi kwa wazee  kumi kwa kuwapa unga, na tumetoa zawadi kwa watoto yatima wawili ya mbuzi kwa kila mototo mbuzi wake, tumetoa zawadi kwa watoto 60 wa shule ya msingi bushiri ya bima ya afya ambayo inamaliza muda wake mwaka 6/12/2018’’. Amesema Mazika.
 
Licha ya kufanya tamasha hilo kwa kugawa zawadi  kwa wanafunzi watoto yatima na kuwasaidia wazee wa kijijini hapo, tamasha hilo pia liliambatana na upimaji wa hiyari wa VVU ambapo katibu huyo amewapongeza kwa kwa uamuzi wao wa kupima kwa hiari.


No comments

Powered by Blogger.