VIJANA WILAYANI PANGANI WASHAURIWA KUJIAJIRI



Vijana waliyani pangani wemetakiwa kujituma na kuacha kulalamikia ukosefu wa ajira, na badala yake wajikite katika shughuli za kujiajiri zitakazoweza kuwaingizia kipato ikiwemo kilimo na biashara.

Akizungumza  katika kipindi cha Makutano kinachorushwa na Panagani Fm, kijana aliyeshinda nafasi ya kwanza katika shindano la kumtafuta kijana bora wa mfano 2017 Bwana Seleman Hamisi kutoka kijiji cha Kimang’a, amesema ili kujikomboa kutoka katika umaskini, vijana wilayani Pangani hawana budi  kujiajiri na kujitosa katika soko la biashara huria.



Aidha Bwana Seleman amewaasa vijana kutokatishana tamaa katika safari ya kuyafikia maendeleo, bali watiane moyo utakaowaongezea ujasiri ili waweze kipiga hatua zaidi ya kuondokana na umasikini unaowakabili.

Kijana Selemani Hamisi ameshinda nafasi ya kwanza kama kijana mwenye mfano wa kuigwa katika jamii, tuzo zinazoratibiwa na shirika la Uzikwasa kutokana na ujasiri wake kukemea vitendo vya ukatili kwa watoto na akinamama, kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii, na uhamasishaji kwa vijana wengine ili wawe kama yeye au hata kumzidi.


No comments

Powered by Blogger.