MAMLAKA YA MAJI PANGANI MJINI YAANZA KUTEKELEZA AGIZO LA MHESHIMIWA AWESSO



Siku moja baada ya agizo la Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mheshimiwa Jumaa Hamidu Awesso kuitaka Mamlaka ya maji Pangani Mjini (PAWASA) kuwa hadi kufikia leo tarehe 5/12/2017 upatikanaji wa maji uwe umetengemaa eneo la Pangani Mjini, hatimae mamlaka hiyo tayari imeanza kuchua hatua za utekelezaji.

Akizungumza na Pangani Fm mapema leo meneja wa maji Pangani Mjini Bwana Adamu Sadick amesema kuwa  wamepokea agizo hilo la Naibu Waziri wa Maji kwa moyo mmoja, na mpaka sasa wanalifanyia kazi na wako katika hatua za mwisho za matengenezo na kuwataka wananchi wilayani Pangani kuwa na uvumilivu juu ya tatizo hilo.

‘’Tumepokea agizo la Mhehsimiwa Naibu Waziri, na mpaka sasa hivi tatizo la maji kwa maeneo ya Pangani Mjini tunalifanyia kazi kwa maana mashine ambayo tunaitegemea kuitumbikiza katika kisima ambacho kimeleta shida ipo katika hatua za mwisho za matengenezo,  kwa hivyo tunategemea kwa siku ya kesho itakuwa imekamilika matengenezo hayo, na pia tunaomba radhi kwa usumbufu unao jitokeza kwa sasa.’’ Alisema Bwana Adamu

Mapema jana Mheshimiwa Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Awesso alitoa agizo kwa mamlaka hiyo  wilayani Pangani kufanya matengenezo ya haraka ili kuondoa usumbufu uliojitokeza wa kukosa maji kwa wakazi wa Pangani Mjini.

No comments

Powered by Blogger.