WANANCHI PANGANI WATAKIWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA KUTEKELEZA MIPANGO INAYOWEKWA NA SERIKALI



Jamii Wilayani Pangani imeombwa kushiriki kikamilifu katika juhudi mbalimbali za kutekeleza mipango inayowekwa na serikali na hata mashirika binafsi kwa ajili ya kupinga mabadiliko ya tabia nchi.

Hayo yamesemwa na katibu tawala mkoa wa Tanga Bi Zena Ahmed Saidi alipohudhuria katika uzinduzi wa mradi wa mabadiliko ya tabia nchi ambapo amesema kuwa, serikali inafanya jitihada za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi hivyo wananchi nao nijukumu lao kuchukua hatua ili kukabiliana na mabadiliko hayo.

'Kwa hiyo katika kukabiliana na hili tumeona serikali imejenga ukuta na nyinyi kama wananchi muelekeze nguvu zenu katika hili suala la upandaji wa mikoko ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi’’ amesema Zena.

Awali akiwasilisha taarifa ya Mradi Afisa kutoka shirika la Climate Action Network Bwana Kelvin amesema kuwa matarajio yao kama CAN ni kuwaongezea wadau uwezo kuhusu namna bora ya kukabiliana na kujenga ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi.

‘’Kuwaongezea wadau kuhusu namna bora ya kukabiliana kujenga ustahamilivu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabia nchi, kupunguza uharibifu na upotevu wa vitu mbali mbali kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, kupunguza uharibifu na upotevu wa vitu mbali mbali nah ii ni kutokana na kikao kilichokaliwa huko Poland kwa ajili ya mpango wa kuwasaidi wananchi wan chi zinazoendelea. Amesema Kelvin.

Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi kumuathiri mwanamke moja kwa moja katibu tawala wa mkoa Bi Zena amelisisitiza shirika la CAN kumtumia kwa asilimia kubwa mwanamke ili waweze kufanikiwa katika mradi wao.

‘’Kwenye mawasilisho yenu mlikuwa mnasema kuwa mwanamke ndio wanaopata shida sana endapo kutatokea mabadiliko ya tabia nchi kwa sababu kama ni maji wao ndo watafuata huduma hiyo kwa umbali zaidi, sisemi kama wakina baba hawaathiriki hapana, sasa kutokana na hilo ni vyema katika hali ya kupambana na mabadiliko haya ya tabia nchi ni vyema mkawashirikishwa wanawake kikamilifu pia msiwasahau wakina baba’’ Amesema Zen.

Mradi huu wa uunganishaji jitihada za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi maendeleo endelevu pamoja na kupunguza umasikini nchini Tanzania, umezinduliwa leo katika wilaya ya pangani na mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miaka 3 katika wilaya mbili za mkoa wa Tanga ambazo ni Lushoto na Pangani pamoja na wilaya ya Chalinze mkoa wa Pwani, huku ikizishirikisha sekta za kilimo, mifugo, uvuvi,  mazingira, ustawi wa jamii, maliasili na nishati.

No comments

Powered by Blogger.