WANAWAKE KIJIJI CHA PANGANI MASHARIKI WATAKIWA KUWEKA KIPAUMBELE KATIKA KUTETEA HAKI ZAO.




Wanawake wa Kijiji cha Pangani Mashariki Wilayani Pangani wametakiwa kuwa kipaumbele katika kutetea haki zao, na kujiona wana uwezo wa kushika nyadhfa mbali mbali za uongozi kwenye Jamii zao.

Akizungumza wakati akiendesha mafunzo ya Jinsia kwa kamati ya kudhibiti Ukimwi, Jinsia na Uongozi VMAC ya kijiji cha Pangani Mashariki, muwezeshaji kutoka shirika la Uzikwasa Bi Salvata Kalanga, amesema wanawake lazima wajitambue na wadai haki zao ili kujiletea maendeleo wao binafsi na jamii nzima kwa ujumla.

 ‘’Tutakapofikia kwenye suala la kudai maendeleo, wanawake lazima tudai haki zetu, hatuko katika zama za kale, kwa hiyo wanawake lazima tufuke maali tuwe na lugha zitakazotufanya tusikilizwe, na ndio maana mafunzo haya hatuyatoi kwa wanawake peke yake, tunawachanganya ili tutembee katika njia moja’’ amesema Salvata.

Nao baadhi ya wanaume waliopo kwenye kamati hiyo walikuwa na mitazamo tofauti kuhusu kumpa uwongozi mwanamke katika nyanja mbali mbali, huku wakisema  wamekuwa wagumu kuwapa wanawake uwongozi kwa sababu ni rahisi kurubuniwa.

‘’Wanawake wamekuwa na udhaifu mwingi sana na hata kwenye kurubuniwa ni raisi, mimi kama mimi katika maisha yangu sitaki mwanamke aniongoze hawa watu hawana misimamo kabisa’’ amesema mmoja wa wanaume hao.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Pangani Mashariki Bwana HAJI NUNDU amewataka wajumbe wanzake kuyathamini mafunzo hayo na kuyapeleka katika jamii zao, ili kuondokana na mikwamo mbali mbali inayowakabili katika jamii yao.

‘’ La msingi na la busara ni kufanya thamani ya mafunzo haya ili tupunguze au kuondoa kabisa suala la unyanyasaji.’’ Amesema HAJI NUNDU
 
Haya yamejiri leo katika siku ya pili ya mafunzo wanayopatiwa wajumbe wa kamati ya kudhibiti Ukimwi, Jinsia na Uongozi ya kijiji cha Pangani Mashariki, mafunzo yenye lengo la kuibua matukio ya ukatili, unyanyasaji kwa wasichana pamoja na wenza ili kuyatafutia ufumbuzi wa pamoja.

No comments

Powered by Blogger.