WAKULIMA PANGANI WATAKIWA KUFUATA USHAURI WA KITAALAMU



Wakulima wilayani Pangani wametakiwa kuzingatia ushauri wa wataalamu wa kilimo ili kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi na kuongeza thamani ya mazao.

Akizungumza na Pangani Fm afisa kilimo wa kata ya MADANGA Bwana Rajabu Kiroka  mbali na kuwataka wakulima kuzingatia ushauri wa kitaalamu, amewashuri kutumia mbegu zinazokomaa kwa muda mfupi na kuwataka wafugaji kupunguza mifugo yao ili iweze kuwa na tija.

‘’Ninachowashauri wakulima kwanza wawe bega kwa began a wataalamu wa kilimo kwa kuwa pamoja na kusikiliza ushauri wa wataalamu kwa kupanda mbegu bora, na kwa wale wafugaji wafuge kwa kutumia ufugaji wa kisasa kwa maana ya kuwa na idadi ndogo ya mifugo ili kuepusha migogoro ya wafugaji’’ Amesema Kiroka.

Kwa upande wake mkulima katika kijiji cha madanga ameeleza kuwa changamoto kubwa ya mabadiliko hayo yanatokana na uharibifu wa mazingira ikiwemo suala la ukataji miti hovyo.

‘’Kiukweli ukataji wa miti umeshamiri sana hasa kwa kata yetu ya madanga na wazee wetu wametuachia minazi lakini hadi sasa imemalizika kabina watu wanakata miti ovyo bila ya kuangalia athari ya baadae ni nini kwa kweli lazima serikali itoe elimu ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi’’ Amesema Arabia.

Mabadiliko ya tabia nchi yamekua miongoni mwa ajenda kuu katika jumuia mbali mbali  za kimataifa ikwemo umoja wa mataifa na jumuiya ya afrika na inasadikiwa kila mwaka watu zaidi 200 huathiriwa na ukame mafuriko ambayo ni matokeo ya mabadiliko ya tabia nchi.

No comments

Powered by Blogger.