WADAU WA MAENDELEO PANGANI WATAKIWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI



Wadau wa Maendeleo katika Nyanja mbalimbali Wilayani Pangani wameaswa kushirikiana kwa pamoja, ili kufikia adhima ya Serikali ya Viwanda kwa kuwa na mifano halisi kiutendaji.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani Bwana SABAS DAMIAN CHAMBASI kwenye Kipindi cha ASUBUHI YA LEO kinachorushwa na kituo hiki, na kuongeza kuwa ili kuijenga Pangani ya viwanda ni lazima wapatikane watu wenye ujuzi na maarifa katika falsafa ya viwanda.

Amesema kuwa wadau bila kubweteka, wanapaswa kuhakikisha wanachukua hatua za makusudi kumuunga mkono Muheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli katika adhma ya serikali yake ya kufikia uchumi wa viwanda.
 
‘’Tunaitaji sasa kuijenga pangani ya viwanda, pangani ya viwanda bila kuwa na watu wenye ujuzi, bila ya kuwa na watu wenye maarifa, na ujuzi hatuta weza, kuna kauli mbiu inayosema mkoa wetu viwanda vyetu, sasa sisi tunasema pangani yetu viwanda vyetu, tuanze kuchukuwa hatua kwa kumuunga mkono rais ya Tanzania ya viwanda, tusibweteke, tuhakikishe tunathubutu kwa kuchukuwa hatua ili tufikie malengo’’ Amesema Sabas.

Bwana SABAS DAMIAN CHAMBASI ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani, amemalizia kwa kuomba ushirikiano baina ya waheshimiwa madiwani, watendaji wote wa halmashauri, taasisi za kiserikali na binafsi na wadau wote wa maendeleo, kuhakikisha wanashikamana iki kuijenga pangani moja kwa nguvu ya PAMOJA.

‘’kwanza niwatake kuwa tuungane waheshimiwa madiwani watendaji wote wa halmashauri, pamoja na wadau wa maendeleo kama vile nmb, uzikwasa, tanesco na taasisi mbali mbali kama bandari na tamesa ili tukakikishe tunaijenga pangani yetu’’ amsema Sabas.

 Leo kupitia kipindi cha ASUBUHI YA LEO Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani Bwana Sabas Damian Chambasi, alikuwa akitoa taarifa za utekelezaji wa mipango mbalimbali tangu alipowasili kiutendaji katika Halmashauri hiyo mwezi wa 7 mwaka 2016 hadi Desember 31-2017, na mipango itakayotekelezwa mwaka huu mpya 2018.

No comments

Powered by Blogger.