JESHI LA POLISI PANGANI LAKIRI KUPUNGUA MATUKIO YA UKATILI, LAKINI LASEMA KAZI BADO!



Kamanda wa jeshi la polisi wilaya ya Pangani bi chritina musiyan hii leo ameelezea kupungua kwa makosa ya vitendo vya ukatili yaliyo ripotiwa kutoka thalathini na tatu kwa mwaka 2016 hadi kufikia thelathini na moja kwa mwaka 2017.

Akizungumza na kituo hiki ofisini kwake Bi Christina amesema kuwa kwa mwaka 2017 waliweza kupokea makosa 31 ambapo makosa nane yakiwa tayari mahakamani huku 2016 makosa 11 yalifikiswa mahakamani kati makosa 33 yaliyoripotiwa.

‘’Mwaka 2017 tuliweza kupokea taarifa za makosa haya yakiwa 31 ambapo makosa nane tayari yalikwisha fanyiwa upelelezi na kufikishwa mahakamani, sita yanaendelea mahakamani katika hatua tofauti na mawili tayari yalikwishafanyiwa maamuzi ya mahakama. Na kwa mwaka 2016, tulipokea jumla ya makosa 33 ambapo makosa 11 yalifikishwa mahakamani na makosa sita yaliweza kuondolewa mahakamani, na hapa kuna upungufu wa makosa 2 kati ya mwaka 2016 na 2017’’ Amesema OCD.

Kamanda Musyani ameongeza kuwa hawezi kusema kuwa makosa ya ukatili Pangani yamepungua kwani utofauti ni mdogo na pia idadi hiyo ni yale matukio yaliyoripotiwa tu kwani bado kwenye jamii matukio yapo ila hayajafikishwa kwenye vyombo vya sheria.

‘’Siwezi kusema kwa toauti ya makosa mawili tuseme ukatili kwa Pangani haupo hapana, hizi tunazozizungumzia ni zile kesi ambazo zimetolewa taarifa kituoni, lakini tujuwe kwamba yapo ambayo tunayasikia kwa mbali lakini kituoni hayajafika na pia hatuwezi kusema kuwa tumefanikiwa kwa sababu bado tatizo lipo katika kaya zetu na katika jamii yetu ya Pangani, utofauti bado ni mdogo sana bado uwelewa na ujasiri wa watu kuja kutoa taarifa kituoni haujafikia lengo na wengine wanakuja kituoni kwa mihemko tu, akishakuja kutoa taarifa hajui bado kama kuna kazi au jukumu la yeye kuja kuthibitisha.’’ Amesema Kamanda Musyani.

Aidha kamanda Musyani amewaomba wananchi kushirikiana na jeshi la Polisi ili kila mtu apate stahiki yake anayotakiwa kuipata kwani mtu anapopewa adhabu stahiki ni kwa ajili ya wengine kujifunza.

‘’Tunaposema kwamba watu washirikiane ili watu wapate adhabu ama hukumu stahiki tunamaanisha kwanza kuifunza jamii na mtu kujifunza, watu wajue kwamba kila mtu anahitaji kuwa huru na kila mtu ana wajibu wa kuitumia haki eneo hili la Pangani au maeneo yoyote ili kila mtu ajifunze’’ Amesema OCD.

Licha ya kuwepo kwa idadi ndogo ya matukio yanayo ripotiwa kituoni hapo bado baadhi ya kesi zimeonekana kukosa ushahidi ambao utawezesha kupelekwa mahakamani jambo ambalo linasababisha kuwepo kwa muda mrefu.

No comments

Powered by Blogger.