KIJIJI CHA KIGURUSIMBA WILAYANI PANGANI CHAFANYIWA MAFUNZO SAIDIZI NA SHIRIKA LA UZIKWASA



Mafunzo ya uongozi wa mguso yanayotolewa na shirika la UZIKWASA  yameelezwa kuwa chachu  iliyosaidia wananchi na viongozi  katika kijiji cha Kigurusimba  kuripoti  matukio ya  ukatili  na unyanyasaji wa kijinsia  yanayojitokeza kijijini  hapo.

Hayo  yameelezwa na wajumbe wa kamati  ya kudhibiti  ya Ukimwi Jinsia na Uongozi wakati wa mafunzo saidizi kwa kamati hiyo ambapo wajumbe hao wamesema kuwa kwa sasa jamii ina mwamko wa kuripoti  matukio hayo.

Nao baadhi ya wajumbe ya kamati  hiyo wameeleza kusikitishwa   na  hatua  ya kuwaona wahalifu wa matukio ya ukatili wakiwa huru mtaani badala  ya kuchukuliwa hatua za kisheria  na kueleza kuwa  hali hiyo  inapunguza ari na hamasa kwa wananchi kufichua matukio hayo.

‘’Kama sisi kwetu Kigurusimba tumewekea mfano jambo ambalo limefanyika hapa majuzi kati hatukuonyeshwa ushirikiano kwamba jambo lile wao limewagusaje kuona kulifuatilia na kulipatia ufumbuzi hata na majibu ya mwisho hakika na ikafanyika hatua yeyote hata sisi ambao tumepeleka taarifa ile tukatiwa moyo kwamba jeshi la polisi linaonyesha ushirikiano na yeyote atakayetoa taarifa. ‘’ Amesema  mmoja wa wajumbe.



Kwa upande  wake  muwezeshaji kutoka  shirika  la UZIKWASA Bwana FILBERT MASHINGIA amewataka  wanakamati  hao  kudumisha ushirikiano na kusema  kuwa ni dhahiri  kuwa kamati  hiyo  itafanya vizuri kwa mwaka huu wa 2018.
 
‘’Ushauri wangu katika kamati ni kwamba kuendeleza zaidi ushirikiano hata wakati tukiwa na majadiliano katika vikundi ushirikiano ni neno mbalo limeibuka sana na wao wameweza kulithamini wakaona kwamba ni kitu muhimu kuhusu ushirikiano kwani mpaka leo kuwepo kwa wajumbe , na baadhi ya wenyeviti mbali mbali hata katika kipindi cha nyuma kwenye mafunzo ya uongozi wa mguso hawakuwepo lakini leo wameweza kuwepo, imeonekana kwamba kuna umuhimu wa wajumbe hawa kuwepo, ushauri wangu katika kamati ni kuendeleza zaidi ushirikaino.’’ Amesema Bwana Mashingia. 

Mafunzo saidizi kwa kamati za kudhibiti  ukimwi VMAC hufanyika  mara  baada ya kamati hizo kupatiwa mafunzo ya uongozi wa mguso.

No comments

Powered by Blogger.