KIFO CHA DIWANI SAIDI MAJIRA CHAACHA SIMANZI HALMASHAURI YA PANGANI



Halmashauri ya Wilaya ya Pangani imeelezwa kusikitishwa na kifo cha aliyekuwa Diwani wa kata Madanga Wilayani humo Ndugu Saidi Majira kilichotokea jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili.

Akizungumza na Pangani fm Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani Muheshimiwa Sefu Ally Mapepo amesema kuwa "Ndugu Majira aliyekuwa akisumbuliwa na matatizo mbalimba ilikwemo mgongo na kiuno alifikishwa Hospitali ya taifa na jana akafariki dunia" ameleza MhSefu ally Mapepo

"Aidha Ndugu Saidi Majira pia alikuwa ni mshauri wa karibu wa Halmshauri kutokana na umahiri wake katika kuongoza kamati mbalimbali, huku ikielezwa kuwa kuondoka kwake kwenda mbele ya haki kumeacha pengo kubwa ndani ya Halmashauri hiyo."ameleza MhSefu ally Mapepo

Marehemu Saidi Majira anatarajiwa kuzikwa hapo kesho majira ya saa saba mchana katika kijiji cha Ushongo, huku wananchi wakitakiwa kuwa na subra katika kipindi hiki kigumu cha kumpoteza mtu muhimu Ndugu Saidi Majira.

Shirika la Uzikwasa na Pangani fm inatoa pole kwa wote walioguswa na msiba huu. Innalillahi wainna ilayhi rajiuun- Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe.

No comments

Powered by Blogger.