WANANCHI WILAYANI PANGANI WATAKIWA KUNYWA DAWA ZA NGIRI MAJI NA MATENDE ILI KUTOATHIRI UKUAJI WA UCHUMI.



Wananchi Wilayani Pangani wameshauriwa kushiriki kikamilifu katika zoezi la unywaji wa dawa za magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, zoezi ambalo limekwishaanza kutekelezwa kwenye maeneo yote wilayani humo.

Akizungumza mapema leo katika kipindi cha ASUBUHI YA LEO kinachorushwa na kituo hiki Mratibu wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Wilayani Pangani Dk Yusuf Makange, amesema kuwa kuendelea kusambaa kwa magonjwa hayo kunaendelea kuathiri uchumi wa nchi kutokana na nguvu kazi kubwa ya taifa kuugua.

‘’Mbwu amekuwa ni msafirishaji wa magonjwa kutoka kwa mtu kwenda kwa mtu mwingine ambapo athari zake mtu anavimba sehemu za siri, anakuwa na tende na matokeo yake anapata ulemavu.’’amesema dokta makange.


Aidha Mratibu huyo wa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele Wilayani Pangani amesema kuwa, Pangani ni miongoni mwa halmashauri tano mkoani Tanga zenye kiwango kikubwa cha maambukizi ya magonjwa hayo, huku akiwaomba viongozi mbalimbali kutumia nafasi zao kuhamasisha wananchi wao ili kufanikisha zoezi hilo.

‘’Halmshauri tano mkoa wa tanga bado tunaendelea na hili zoezi kwa sababu maambukizi yapo juu, kwa hali hiyo ndo mana tunasisitiza kuwa viongozi waliokuwepo katika ngazi nikimaanisha mwenyekiti wa kijiji hadi viongozi wote maarufu tunaomba ushirikiano katika hili ili kuondoa maambukizi’’amesema dokta makange.



No comments

Powered by Blogger.