WALIMU SHULE YA MSINGI MIKINGUNI WILAYANI PANGANI WAASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII



Wito umetolewa kwa walimu wa shule ya msingi MIKINGUNI wilayani pangani kufanyakazi kwa bidii na kujitolea kwa moyo wa kuwafundisha wanafunzi ili waweze kuwa chachu ya mafanikio katika kijiji cha MIKINGUNI wilayani humo.

Hayo yamezungumzwa na mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo bwana WAZIRI MBEZI na kuongeza kuwa wazazi wasiwaozeshe watoto wakiwa na umri mdogo wawaache wasome kwanza hayo mambo mengine yatafuata baadae.

’wazazi wamekuwa na tabia ya kuwalimbikia watoto wa kike kazi za nyumbani hii haisaidii kunyanyua motto huyu kielimu, hapo hapo atakapo fanya vibaya ndo mzazi unakuwa kipaimbele kumuozesha, tunatakiwa kubadilika wanamikinguni’’ amesema mbezi.

Bwana WAZIRI amesema kuwa mkwamo uliopo ni utoro kwa wanafunzi jambo linaloitaji ushirikiano kati ya walimu na wazazi ili kuuondoa.

’Kwa mwaka huu wa 2017 matokeo angalau yametoka mazuri, lakini mkwamo uliokuwepo ni swala la utaro wa reja reja kwa wanafunzi, naamini tukishirikiana kati ya walimu na wazazi ili swala litaondoka’amesema bwana waziri

No comments

Powered by Blogger.