VIJANA WASHAURIWA KUJIUNGA VIKUNDI ILI KUANZISHA MIRADI




Ziara ya mwenyekiti wa kijiji cha Boza  kwa ajili ya elimu kwa wanchi juu ya namna ya kujiunga katika vikundi mbalimbali vya kimaendeleo na ujasiriamali imeanza jana katika kitongoji cha Choba.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa kijiji cha Boza,Bwana Shabani Sufiani Musa na kuwataka wakazi wa kijiji cha Choba kuwa katika vikundi kwa ajili ya kupewa mikopo ili kujiendeleza kiuchumi kwani hakuna fedha yoyote ambayo serikali itaitoa kwa mtu mmoja pekee.

‘’Na mradi ambao mtaubuni hakikisheni mnaandika na mahitaji yake ili mpate pesa kulingana na namna ambavyo mnaweza kuuendesha,”tena sasa kuna wengine wamesema hapa kwamba kipindi cha nyuma mlikuwa mnapewa pesa ambazo haziendani na mahitaji sasa niwaambie kitu kimoja sasa hivi haitakuwa kama zamani mtu aomba milioni moja anapewa laki mbili”alisema Shabani Sufian mussa.

Kwa upande mwingine afisa uwezeshaji wanachi kutoka halmashauri ya wilaya ya Pangani Bi Ester John amewataka wanachi hao kuhudhuria katika semina juu ya mafunzo ya ujasiriamali ambayo itafanyika katika kijiji cha kimang’a tarehe 18 mwezi novemba mwaka huu 2017.
Semina hiyo itaendeshwa na wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwemo SIDO,watu wa benki akiwamo pia mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Zainabu Abdallah Issa.

Kijiji cha Boza kina vitongoji kama vile choba,mnazi mmoja,kibaazi na Boza,ambapo ziara hiyo ni ya siku tatu,na huu ni utaratibu ambao mwenyekiti huyo amejiwekea utaratibu wa kuzungumza na wanachi wake kwa ajili ya kutoa mrejesho juu ya masuala ya uongozi na kuona namna gani ya kutataua kero za wanachi.

No comments

Powered by Blogger.