UBAGUZI BAINA YA WAZAWA NA WAGENI WASEMEKANA KUKWAMISHA MAENDELEO MKOANI TANGA



Jamii Mkoani Tanga imetakiwa kuacha tabia ya kibaguzi inayowagawa wazawa na wageni, badala yake washirikiane na kuwa kitu kimoja katika shughuli za kimaendeleo.

 Wakitoa maoni yao katika kipindi cha ASUBUHI YA LEO kinachorushwa na kituo cha Pangani fm Radio, wachangiaji kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Tanga, wamesema tabia hiyo ya kibaguzi ipo katika maeneo mbalimbali ya nchi, huku wakisema tabia hiyo haifai kwani maendeleo ya wilaya, mkoa na taifa ni jukumu la kila mmoja.

“Tunanyanyaswa kisa sisi hatujazaliwa hapa, sio vizuri sisi ndio tunaleta chachu ya mabadiliko ya iuchumi halafu wanatutenga, tukifanyikiwa kisa wageni wanatuibia si utanzania huu, sisi tunahangaika kwa kuwa tunajua maendeleo ya wilaya zetu, mikoa yetu na  nchi yetu ni jukumu la kila mmoja” wamesisitiza baadhi ya wachangiaji.

Aidha wachangiaji hao wamesema kuwa ubaguzi huo unaoendelea katika baadhi ya maeneo ya nchi, unaendelea kuwanyima baadhi ya watu na kuwaweka tofauti watanzania jambo ambalo si utamaduni wa taifa hili.
“Mtanzania si mgeni katika eneo lolote la taifa hata kama hajazaliwa eneo hilo, anazohaki zote na anastahili kuzipata kama watanzania wengine aliowakuta eneo hilo. Kwanini wanatugawa ndio utanzania huo” wameendelea kusisitiza.

Katika hatua nyingine wachangiaji hao wameongeza kuwa ni vyema serikali ikajiweka karibu zaidi na jamii, ili kujua masuala mbalimbali yanayowasibu watanzania kila siku.

No comments

Powered by Blogger.