AENDA JELA KWA KUMUIBIA MKE WAKE WILAYANI PANGANI



Mahakama ya mwanzo mwera imetoa hukumu kwa kijana LUKAS ATHUMAN (29) kwenda jela miezi mitano (5) kwa kukutwa na hatia ya kuvunja na kuiba godoro moja na mashuka mawili, mali ya mke wake Bi Amina Abdallah.

Hati ya mashtaka inaeleza kuwa kijana Lukas mnamo  tarehe 30/6/2016 kijiji cha Kasanga wilayani Pangani, alitenda kosa la kwanza ambalo ni kuvunja nyumba kwa nia ya kuiba, na kosa la pili kuiba godoro moja la futi tano kwa sita pamoja na mashuka mawili mali zenye thamani ya shilingi laki moja na elfu ishirini.

Inadaiwa kuwa kijan Lukas alivizia mke wake huyo alipokuwa amekwenda katika mizunguko yake ya kila siku majira ya saa 5:00 usiku na kutekeleza tukio hilo.

Tarehe 21/7/2016 mahakama ya mwanzo Mwera chini ya Hakimu ANTONY HAMZA ilimuhukumu kijana Lukas kutumikia kifungo cha nje miezi mitano ambapo alitakiwa kufanya usafi wa maeneo ya zahanati na mahakama.

No comments

Powered by Blogger.