KIJANA AENDA JELA KWA KUMTISHIA MTU MAISHA WILAYANI PANGANI



Mahakama ya mwanzo kata ya Mwera wilayani Pangani imemhukumu kijana MOHAMED YASSIN (21) kwenda jela miezi kumi na mbili (12) kwa kosa la kumtishia kwa silaha Bwana ABDALAH SHABAN.

Hati ya mashtakaowasilishwa mahakamani hapo ili inaeleza kuwa mnamo tarehe 16/8/2017 majira ya saa nane kamili mchana mshtakiwa alitaka amchome kisu Bwana Abdalah Shabani ambacho alikuwa amekiweka  kwenye mfuko wa nguo alizokuwa amezivaa.

Baada ya mshtakiwa kusomewa shtaka hilo alikataa kuhusika katika tukio hilo na ndipo mahakama ikasikiliza ushahidi wa pande zote mbili na kumkuta mshtakiwa na kosa  lililopelekea kuhukumiwa kwenda jela miezi 12.

Kijana MOHAMED kabla ya hapo alikuwa akitumikia kifungo cha miezi tisa (9) jela kwa kosa la kutoroka chini ya ulinzi halali wa askari wa kituo cha polisi Kipumbwi, kwa kuvunja dirisha la lock up.

No comments

Powered by Blogger.