UONGOZI WA KATA YA KIMANG'A WILAYANI PANGANI KUFANYA KIKAO NA WAGANGA WA JADI



Uongozi wa kata ya Kimang’a wilaya ya Pangani kesho unatarajiwa kufanya kikao na waganga wa jadi ili kujadili masuala mbalimbali yanayohusu taaluma zao pamoja na kuwatambua kisheria.

Akizungumza na Pangani Mm Afisa mtendaji wa kata hiyo Bwana Salimu Ugendo Athumani, amesema kuwa wameamua kuitisha kikao na waganga hao ili kuwaelimisha juu ya sheria na utaratibu zinazowahusu katika kazi zao.

Katika hatua nyingine Bwana Ugendo amesema, endapo watawaelimisha na kuwasijili waganga hao, itasaidia kuzingatia uhalali wa njia na kazi zinazofanywa na kwa kila mgang.

Mbali na waganga wa jadi wenye, kikao hicho pia kinatarajiwa kuhusisha, Afisa Utamaduni, Mratibu wa Waganga wa Jadi Wilaya ya Pangani pamoja na viongozi wengine wa kata hiyo

No comments

Powered by Blogger.