BODA BODA PANGANI WALALAMIKIA ABIRIA WAO KUKATAA KUVAA HELMET



Kutokana na kuwekwa utaratibu wa kila Boda Boda kuwa na kofia ngumu mbili,  baadhi ya waendesha vyombo hivyo wilayani Pangani wameiomba serikali kupitia jeshi la polisi pamoja na kitengo cha Afya kutoa elimu kwa abiria juu ya umuhimu na jinsi ya kutumia  kofia hizo bila kupata madhara.

Wakizungumza na Pangani Fm Baadhi ya waendesha Boda Boda wa mjini Pangani wamesema tangu kuwekwa utaratibu huo asilimia kubwa ya waendesha Boda Boda wameitikia wito huo wa kuwa na kofia mbila lakini changamoto wanayoipata ni baadhi ya abiria kukataa kuvaa kofia hiyo wakihofia usalama wa afya zao.

Aidha waendesha Boda Boda hao wameliomba jeshi la polisi kukaa na kujadili kwa kina kuhusu matumizi ya kofi mbili kutokana na changamoto wanazokutana nazo.

Utaratibu wa kila Boda Boda kuwa na kofia ngumu mbili lilitolewa miezi miwili iliyopita  na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Mheshimiwa Mwigulu Nchemba  wakati akiongea na madareva wa Boda Boda mkoani Shinyanga ambao walipatiwa  mafunzo ya usalama barabarani mkoani humo ambapo amewataka polisi kuwakamata madereva hao endapo hawatatii agizo hilo.

No comments

Powered by Blogger.