BOTI YA UVUVI YAZAMA NA KUUA MTU MMOJA WILAYANI PANGANI HUKU WENGINE WANNE HAWAJULIKANI WALIPO




Mtu mmoja amefariki dunia na wengine wanne hawajulikana walipo mara baada ya chombo walichokuwa wakikitumia katika shughuli za uvuvi kupata dhuruba katika mkondo wa bahari ya hindi wilayani Pangani.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo afisa mpelelezi kutokea wilayani Pangani ASP Matiku amemtaja aliefariki dunia kuwa ni Jumanne Abdallah mwenye umri wa miaka 18.

“Aliyefariki ni mkazi wa Shakani huko Zanzibar, lakini pia mpaka sasa watu waliookolewa ni 12 ambao wamethibitishwa, nah ii imetokana na dhoruba kubwa ya mawimbi baada ya bahari kuchafuka, matokeo yake chombo chao kikapigwa wimbi na kuzama” alisema Matiku.

Matiku ameongeza kwa kusema kuwa, amezungumza pia na mmiliki wa chombo hicho Bwana Mohammed Mzee, na kulieleza jeshi la polisi kuwa jumla ya watu waliokuwepo ndani ya chombo hizho ni 17.

Aidha asp Matiku amesema kuwa jeshi la polisi bado linaendelea kuwatafuta watu wanne ambao wajaonekana na kuitaka jamii kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo ili kukamilisha zoezi hilo

No comments

Powered by Blogger.