'SIKU YA MTOTO WA KIKE DUNIANI' WATOTO WA KIKE WILAYANI PANGANI WATOA NENO!



Wananchi wilayani Pangani wameungana na mikoa mingine kuadhimisha siku ya mtoto wa kike duniani ambapo mambo mbali mbali yamejadiliwa katika majukwaa ya uwezeshaji watoto hao ikiwemo suala la kuwapatia muamko wa kielimu.

Wakizungumza na Pangani Fm baadhi ya watoto wa kike waishio wilayani humo wamesema kuwa, wao kama watoto wa kike wanapaswa kupatiwa haki zao za msingi ikiwemo elimu, kulindwa na kupatiwa malezi bora yatakayo wawezesha kutimiza ndoto zao.

Aidha watoto hao pia wamewataka wazazi na walezi kuweka uwiano sawa katika majukumu kati ya mtoto wa kike na mtoto wa kiume ili wapate muda wa kujisomea huku wakiwaasa vijana wanaojiingiza kwenye mahusiano na wanafunzi wa kike waache kwani wanashindwa kutimiza ndoto zao.

Siku ya mtoto wa kike duniani huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 11/10  ambapo kwa mwaka huu wa 2017 kauli mbiu ya siku hiyo inasema kuwa ‘’KUTOKOMEZA MIMBA ZA UTOTONI KUELEKEA TANZANIA YA VIWANDA’’

No comments

Powered by Blogger.