KAMATI ZA VMAC WILAYANI PANGANI ZATAKIWA KUKAMILISHA MIPANGO KAZI YAO



Kamati za kudhibiti Ukimwi Jinsia na Uongozi VMAC Wilayani Pangani ambazo bado hazijakamilisha utekekezaji wa mipango kazi yao, zimetakiwa kuutumia muda uliosalia kukamilisha kabla ya kuingia kwenye kilele cha Shindano la kutafuta kamati bora kwa mwaka 2017.

Akizungumza na Pangani fm Muwezeshaji kutoka shirika la Uzikwasa Bi Salvata Kalanga, amesema zoezi la ufuatiliaji na tathmini linalofanywa na shirika la uzikwasa, limetoa taswira ya namna kamati hizo zinavyotekeleza mipango kazi yao, huku akizitaka kamati ambazo bado hazijakamisha utekelezaji wake kutokana na vikwazo mbalimbali kutokata tamaa, na badala yake kutafuta njia mbadala ya kutatua vikwazo hivyo.

Pia Bi Salvata amesema moja ya changamoto iliyoibuliwa na wajumbe wa kamati hizo ni kusimamishwa kwa watendaji wa vijiji, ambapo amewataka wajumbe kuacha kulaumu, badala yake kupata funzo jipya kwa lengo la kuisimamia kamati ipasavyo ili kuleta maendeleo kwenye maeneo yao.

Katika hatua nyingine kamati ya Kudhibiti Ukimwi Jinsia nna Uongozi ya kijiji cha Masaika, imesema imefanikiwa kudhibiti tatizo la mimba Mashuleni, kwa kudhibiti watoto kuingia katika mabanda ya video.

No comments

Powered by Blogger.